• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Ujenzi
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu, na Usimamizi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RC SANARE AWAPONGEZA WADAU KWA KUFANIKISHA UKARABATI WA SHULE YA MSINGI MJI MKUU MANISPAA YA MOROGORO

Posted on: February 21st, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Loata Sanare,  amewapongeza wadau kwa kufanikisha ukarabati wa madarasa chakavu katika shule ya Msingi Mji Mkuu iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya ,Morogoro.

Pongezi hizo amezitoa  wakati wa ukaguzi wa madarasa Manne chakavu yaliyokarabatiwa chini ya ufadhili ambapo madarasa mawili yametokana na ufadhili wa Mhe. Abdulaziz Abood Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini kupitia mfuko wa jimbo na mengine mawili chini ya ufadhili wa Nashela Hotel.

Katika ukarabati wa madarasa hayo , Mfuko wa Jimbo la Morogoro Mjini uliweza kuchangia shilingi Milioni 3 na laki 6 na fedha binafsi kutoka kwa Mhe. Abood ni shilingi Milioni 1 na Laki 4 huku ufadhili wa Nashela Hoteli ukitumia takribani shilingi Milioni 10.

"Napenda kutoa pongezi zangu za shukrani kwa wadau wote, haswa Mhe. Abood na Nashela Hotel, kwakweli shule hii ipo barabarani njiani kabisa nilipiga kelele lakini leo angalau ilifikia wakati nikamwambia Mkuu wa Wilaya tuifunge shule hii wanafunzi na walimu tuwahamishe lakini sasa inaonekana kufufuka , niombe Manispaa iangalieni shule hii kwa jicho la huruma ikiwezekana tafuteni pesa haraka kukoa jahazi hali sio nzuri viongozi wanapita njia hii ni aibu kubwa " Amesema Sanare.

Amesema mikakati yake ni kuhakikisha Watoto wote waliofaulu wanaenda shule na wanakaa kwenye madawati na atazunguka kila kata kuona hali ilivyo.

Pia ameendelea kusisitiza kwamba wale walimu Wakuu waliodumu muda mrefu bila ya matokeo mazuri ya ufaulu watashushwa vyeo na kuwa walimu wa kawaida.

Aidha , amesema Walimu ambao hawako shuleni bila taarifa za msingi wakatwe mishahara yao pamoja na kuchukuliwa hatua za kinidhamu.

Pia amewaagiza Maafisa elimu wasaidiane na Wadhibiti ubora wa elimu ili kuleta matokeo chanya ya viwango vya ufaulu katika Mkoa wa Morogoro.

"Tunachotaka ni matokeo, yapo malalamiko mengi shuleni wananchi wanaonewa wakati Serikali ilishatoa maelekezo lakini hayatekelezwi, hivyo hatutakuwa tayari kuwaadhibu wadhibiti ubora wakati wapo waratibu wa elimu, niwaombe waratibu wa elimu wasimamie shule na sitotaka kusikia malalamiko kwani kikwazo cha kwanza katika kuchangia matokeo mabaya ya elimu ni watendaji "Ameongeza RC Sanare.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonjo, ameuagiza uongozi wa Kata ya Mji Mkuu kuhakikisha wanaitisha Vikao vya kuongea  na Wananchi wao kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya elimu na katika vikao hivyo wawashirikishe Mkuu wa Wilaya, Meya na Mkurugenzi ili watoe hamasa.

Amewataka waalimu na watendaji kuhakikisha kila mtu anafanya majukumu kwa nafasi yake huku akiwataka watendaji pamoja na maafisa elimu kuhakikisha kila kinachoingia na kutoka wakisimamie kwa misingi ya sheria na kanuni.

Katika ukarabati wa madarasa chakavu  , utengenezaji huo ulihusisha marekebisho ya sakafu, ukarabati wa kuta za ndani na nje (plasta), ubadilishaji wa silingi bodi (ceiling board), kenchi, uezekaji wa paa jipya, upigaji rangi wa madarasa mawili, wiring na umeme kwenye madarasa mawili pamoja na taa za kuongeza ulinzi mbele na nyuma ya madarasa.

Matangazo

  • HERI YA SIKUKUU ZA CHRISTMAS NA MWAKA MPYA WA 2021 December 24, 2020
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA WATENDAJI WA MITAA DARAJA LA TATU TAREHE 20/6/2020 June 12, 2020
  • TANGAZO LA UCHAGUZI MKUU October 20, 2020
  • TANGAZO KWA WAFANYABIASHARA WANAOTAKA KUPANGA VIOSKI MANISPAA YA MOROGORO March 25, 2020
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • MANISPAA MOROGORO YAIBUKA KINARA WA LISHE MKOA WA MOROGORO

    February 05, 2021
  • WANANCHI WATAKIWA KUENDELEA KUSHIRIKI KATIKA UJENZI WA MADARASA

    January 28, 2021
  • WAITARA ARIDHISHWA NA USAFI MANISPAA YA MOROGORO, ATAKA KASI IONGEZWE KATIKA UPATIKANAJI WA DAMPO LA KISASA

    January 25, 2021
  • MEYA KIHANGA AWACHARUKIA WAALIMU WAKUU, AWATAKA WAJITATHIMINI

    January 19, 2021
  • Angalia Yote

Video

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI MANISPAA YA MOROGORO WAZIRI KOMBO ATANGAZA MATOKEO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA ULIOFANYIKA NOV.24/2019.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa